Wito wa kuunga mkono kura ya Voice waongezwa katika siku ya National Sorry Day

LINDA BURNEY VOICE PRESSER

A tshirt logo reads ‘Voice Makarrata’ at a press conference after the introduction of a bill to establish an Aboriginal and Torres Strat Islander Voice in the House of Representatives at Parliament House in Canberra, Thursday, March 30, 2023. (AAP Image/Lukas Coch) NO ARCHIVING Source: AAP / LUKAS COCH/AAPIMAGE

Miaka sita baada ya kutangazwa kwa Kauli ya Uluru kutoka moyoni, viongozi wa jamii ya kwanza na serikali kwa mara nyingine wame toa wito kwa kuanzishwa kwa sauti yawa Aboriginal na wanavisa wa Torres Strait bungeni kupitia mafanikio katika kura ya maoni.


Katika siku yakitaifa ya Sorry Day na maadhimisho ya sita ya Kauli ya Uluru kutoka Moyoni, viongozi wa jamii za kwanza walijumuika katika Wilaya ya Kaskazini, ambako wali waomba wa Australia waunge mkono kura ya maoni ya Sauti yawa Australia wa kwanza Bungeni.

Siku ya kitaifa ya Sorry Day hukumbuka unyanyasaji ambao wa Aboriginal nawatu wa visiwa vya Torres Strait waliyo pitia, na ilifanywa kwa mara ya kwanza kwenye maadhimisho ya mwaka wa kwanza wa ripoti ya Walete Nyumbani 1998.

Ripoti hiyo ya 1997 ilijiri kupitia uchunguzi wa serikali kwa sera za zamani ambazo, zilisababisha watoto kuondolewa kwa nguvu kutoka familia na jamii zao, kundi la watoto hao lili batizwa jina la vizazi vilivyo ibwa.


Share