Taarifa za habari 19 Mei 2020

Bango la taarifa za habari za dunia la SBS

Bango la taarifa za habari za dunia la SBS Source: SBS

Australia yachunguza uwezekano wakufungua masoko mengine kwa wazalishaji wa mtama, baada ya China kutangaza inawekea mauzo ya mtama wa Australia ushuru wa 80% kwa muda wa miaka mitano ijayo.


Ufaransa na Ujerumani zapendekeza kuanzishwa kwa mfuko wa euro bilioni 500 wa kufadhili juhudi za kuukwamua uchumi wa Umoja wa Ulaya ulioathiriwa na mgogoro wa virusi vya corona.

Serikali ya Tanzania imeondoa zuio la ndege za kawaida za abiria kuingia na kutoka nchini humo ili kuruhusu shughuli za usafiri wa anga na utalii kuendelea kama kawaida.

Thomas Thabane ametangaza kuwa atajiuzulu kama waziri mkuu wa Lesotho kufuatia miezi kadhaa ya shinikizo baada ya kutajwa kama mshukiwa katika mauaji ya aliyekuwa mkewe.

 


Share