Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) amesema kuwa anamatumaini janga la corona litakomeshwa ndani ya miaka miwili.
Mwanasiasa mashuhuri wa upinzani wa Russia Alexei Navalny ambaye yuko mahututi baada ya tuhuma za kuwa alipewa sumu, amewasili katika mji mkuu wa Ujerumani, Berlin, Jumamosi asubuhi kwa ndege maalum, ambako atapatiwa matibabu katika hospitali kuu mjini hapo.
Ujumbe maalum wa Jumuia ya Uchumi ya Afrika Magharibi, ECOWAS, ukiongozwa na Rais wa zamani wa Nigeria Goodluck Jonathan umewasili mjini Bamako, Mali kukutana na viongozi wa baraza la kijeshi lililomlazimisha Rais Ibrahim Boubacar Keita kuachia madaraka na serikali yake mapema wiki hii.