Shirika la GLAPD lawafungulia milango walio athiriwa na COVID-19

Shirika la GLAPD Int'l latoa msaada wa vyakula kwa walio poteza kazi zao

Viongozi washirika la GLAPD Int'l wakiwa pamoja na wanachama walio pokea msaada wa vyakula, wakati wa janga la Coronavirus Source: SBS Swahili

Janga la Coronavirus limesababisha madhara makubwa, kwa baadhi yawahamiaji na wanafunzi wakimataifa wanao ishi nchini Australia.


Wengi wao wamepoteza ajira zao kwa sababu ya janga hilo, na wengine wamekwama nchini Australia baada ya mipaka kufungwa kudhibiti usambaaji wa maambukizi hayo katika jamii.

Viongozi wa shirika la GLAPD walipokea maombi mengi ya msaada kutoka kwa jamii, hali ambayo ilisababisha wazindue mradi wakutoa vyakula na misaada mingine kwa watu ambao wamepoteza kazi na wanakabiliwa na changamoto zakumudu maisha yakila siku, katika mradi wakujaza mifuko ukarimu.

Share