Jean D'amour "nikama nimezaliwa upya".

Mfanyakazi wa duka akagua cheti cha chanjo cha mteja mjini Sydney, Jumatatu, Oktoba 11, 2021

Mfanyakazi wa duka akagua cheti cha chanjo cha mteja mjini Sydney, Jumatatu, Oktoba 11, 2021 Source: AAP

Wakaaji jimboni NSW wameishi chini ya amri zakubaki ndani za Uviko-19 kwa zaidi ya siku 100, ila viongozi jimboni humo wali wapunguzia vizuizi baadhi ya wakaaji ambao wame pata chanjo kamili za Uviko-19.


Maelfu ya wakaaji wa NSW walio kuwa wame pata chanjo zote mbili za Uviko-19 walitazamia Jumatatu 11 Oktoba 2021, ambayo ilikuwa imebatizwa jina la "siku ya uhuru" kwa hamu sana. Hiyo ni siku ambayo wangeweza kutana namarafiki na jamaa wao tena pamoja nakupata huduma zote walizo kosa kwa zaidi ya siku 100.

Bw Jean D'amour ni mmoja wa wakaaji wa Sydney, ambao walikuwa wakisubiri siku hiyo ya ''uhuru'' kwa hamu, alizungumza na Idhaa ya Kiswahili ya SBS masaa machache baada ya watu walio kuwa wame pata chanjo zote mbili kuanza kujumuika katika jamii.

Bonyeza hapo juu kwa taarifa kamili.


Share