Je muhula ujao utafananaje shuleni?

Mwalimu wa sekondari na wanafunzi darasani

Mwalimu wa sekondari na wanafunzi darasani Source: Getty Images

Serikali ya jimbo la New South Wales imetangaza kuwa wanafunzi watarejea darasani muhulu huu, ila itakuwa kwa siku moja au siku mbili kila wiki tu.


Tangazo hilo limejiri baada ya serikali kuzingatia kuendelea kupungua kwa visa vya coronavirus jimboni.

Hili ni tangazo jipya kutoka kwa kiongozi wa jimbo kuhusu, jinsi watakavyo warejesha wanafunzi shuleni, hatua ambayo inatofautiana nchini kote. Ila hatua hiyo inasababisha hali yakuchanganikiwa miongoni mwa wazazi na walimu, ambao wanataka mwelekeo wa umoja.

Viongozi wote wamajimbo nchini wamekiri kuwa mipango yao, inaweza badilika wakati wowote.

Na unaweza pata taarifa mpya kuhusu janga la Coronavirus kwenye tovuti hii: sbs.com.au/Coronavirus.


Share