Hatimae Melbourne yaibuka kutoka vizuizi vya muda mrefu zaidi duniani

Wateja wachangia chakula nje ya mgahawa katika mtaa wa Degraves Street, baada ya Melbourne kuondoka katika vizuizi vya muda mrefu zaidi duniani.Ijumaa 22 Okt 21

Wateja wachangia chakula nje ya mgahawa katika mtaa wa Degraves Street, baada ya Melbourne kuondoka katika vizuizi vya muda mrefu zaidi duniani.Ijumaa 22 Okt 21 Source: AAP

Sherehe za krismasi na mwaka mpya nikama ziliwasili mapema mjini Melbourne, ambao ulikuwa umejipa rekodi yakipekee yakuwa na viuzizi vya Uviko-19 vilivyo dumu kwa muda mrefu zaidi duniani.


Bw Habib Chanzi ndiye mwenyekiti wa Jumuiya yawatanzania wanao ishi jimboni Victoria, katika mazungumzo maalum punde baada yavizuizi hivyo kuondolewa, ali eleza Idhaa ya Kiswahili ya SBS hisia zake baada yakupewa uhuru ambao yeye nawakaaji wenza wa Victoria wametamani kwa muda mrefu.

Bw Chanzi aliweka wazi pia changamoto ambazo viongozi wenza na mamlaka husika, wanakabili kuhakikisha jamii zinaendelea kuwa salama wakati baadhi ya watu wame anza kufurahia uhuru wao mpya, na wakati huo huo mamlaka wanaripoti ongezeko ya idadi kubwa ya maambukizi ya Coronavirus kila siku.

Bonyeza hapo juu kwa taarifa kamili.


Share