Shinikizo ya gharama yamaisha yafanya wanafunzi wasajiliwe katika shule za umma

La Auburn North Public School

Source: SBS

Mwaka wa shule wa 2025 ume anza hii leo Jummanne 28 Januari katika majimbo ya Queensland na Kusini Australia, wanafunzi wa shule za msingi na upili wanatarajia kurejea shuleni kesho Jumatano 29 Januari katika jimbo la Victoria na Wilaya ya Kaskazini.


Katika wilaya ya Australian Capital Territory wanafunzi watarejea shuleni Jumatatu 3 Februari, na katika jimbo la Magharibi Australia wanafunzi watarejea shuleni tarehe 5 Februari.

Nao wanafunzi katika majimbo ya Tasmania na New South Wales watarejea shuleni Alhamisi 6 Februari.

Wakati huo huo janga la gharama ya maisha lina endelea kuweka shinikizo kwa familia zinazo lipa karo ya shule.

Sasa, utafiti mpya umefichua ambako baadhi ya sehemu ghali zakusomea nchini Australia zilipo na ambako familia zinaweza mudu.

Share