Trump na mkewe wapatwa na COVID-19

Siku mbili baada ya mdahalo wakwanza wa kampeni ya urais, Rais wa Marekani amethibitisha kuwa yeye pamoja na mkewe, wamepatwa na Coronavirus.

Donald Trump na mkewe Melania Trump

Rais wa Marekani Donald Trump na mkewe Melania Trump, wathibitishwa kupata Coronavirus Source: AAP

Bw Trump alithibitisha taarifa hizo kupitia mtandao wa Twitter, taarifa hizo zikijiri masaa machache baada ya taarifa kusambaa, kuwa msaidizi wake wa karibu Hope Hicks ame patwa na Coronavirus.

Bw Trump ame andika katika ukurasa wake wa Twitter kuwa, "yeye pamoja na mkewe watasalia katika karantini ndani ya ikulu", ambako ataendelea kuongoza serikali.

Tutawapasha taarifa za ziada, punde tutakapo zipokea.


Share

Published

Updated

By Gode Migerano
Presented by Gode Migerano
Source: SBS Swahili

Share this with family and friends