Taarifa mpya kuhusu COVID-19: Victoria yawasilisha mageuzi ya janga, Queensland kuwakaribisha tena wanafunzi wakimataifa

Hii ni taarifa mpya kuhusu Coronavirus nchini Australia kwa 26 Oktoba 2021.

Wanafunzi watembea katika chuo cha Queensland mjini Brisbane.

Wanafunzi watembea katika chuo cha Queensland mjini Brisbane. Source: Getty Images

 

  • Victoria yawasilisha mageuzi mapya ya afya ya umma kwa hali ya janga
  • Queensland yatangaza mipango kwa wanafunzi wakimataifa
  • NT yalenga 'kutokuwa na sera ya karantini’
 


 

Victoria

 

Victoria inawasilisha sheria mpya za janga bungeni wakati jimbo hilo limerekodi kesi mpya 1,510 za maambukizi ya UVIKO-19 na vifo vinne.

 

Kiongozi wa jimbo atakuwa na uwezo wakutangaza janga baada yakuzingatia ushauri, wa maafisa wakuu wa afya na timu ya afya ya umma.

 

Waziri wa Afya Martin Foley amesema sheria hizo zitakuwa mbadala ya mfumo wa sasa, ambako mipangilio ya hali ya dharura inahitaji tathminiwa na, kuongezwa na waziri kila wiki nje. 

 

Mpango mpya wa masharti kwa adhabu ulitangazwa pia, ambako watu wanao kabiliwa na magumu kifedha wanaweza omba kiwango cha adhabu zao zipunguzwe.

 

Victoria inatazamia kufunguliwa tena Ijumaa, Oktoba 29 wakati jimbo hilo linatarajiwa kufikisha lengo la 80% ya chanjo.

 

Queensland

Kiongozi Anastasia Palaszczuk ametangaza kuwa wanafunzi wakimataifa wataweza rejea jimboni humo katika mwaka wa 2022, jimbo hilo linapo rekodi kesi mbili mpya za maambukizi, zote mbili zikizingatiwa kuwa na hatari ndogo.


New South Wales

New South Wales imerekodi kesi mpya 282 za maambukizi mapya pamoja na kifo kimoja.

 

Jimbo hilo limetoa chanjo kamili 85% kwa umma wenye miaka 16 na zaidi.

 

Pata hapa kilicho karibu yako.

Hali ilivyokuwa nchini Australia katika masaa 24 yaliyo pita

  • ACT imerekodi kesi mpya 12 za coronavirus.
  • Wilaya ya Kaskazini inalengo 'lakutokuwa na sera ya karantini', kwa watu ambao wamepata chanjo kamili kuanzia Januari 18.
 

 


 

Karantini, safari, zahanati za vipimo na malipo ya janga

Karantini na masharti yavipimo husimamiwa nakutekelezwa na serikali zamajimbo na wilaya:

ACT  na 
Kama unataka safiri ng'ambo, unaweza omba kibali mtandaoni.  kwa taarifa zaidi kuhusu masharti yakuondoka Australia. Kuna hatua za mpito kwa safari zakimataifa ambazo hutathminiwa mara kwa mara na serikali, nakuchapishwa kwenye tovuti ya .



Tazama rasilmali zilizo tafsiriwa za huduma yamawasiliano ya shirika la afya ya tamaduni nyingi ya NSW:


Zahanati za vipimo katika kila jimbo na wilaya:

 
 

Taarifa kuhusu malipo ya janga katika kila jimbo la wilaya:

 
 

Share
Published 26 October 2021 2:14pm
By SBS/ALC Content
Presented by Gode Migerano
Source: SBS


Share this with family and friends