Taarifa mpya ya COVID-19: Rekodi mpya ya kila siku kwa NSW wakati chanjo ya Moderna yapewa idhini ya muda

Hii ni taarifa mpya kuhusu Coronavirus nchini Australia kwa leo 10 Agosti 2021.

Watu wakufanya usafi waingia ndani ya shule ya umma ya Bondi Beach, Bondi, Sydney, Jumanne, 10 Agosti, 2021

Watu wakufanya usafi waingia ndani ya shule ya umma ya Bondi Beach, Bondi, Sydney, Jumanne, 10 Agosti, 2021 Source: AAP Image/Dan Himbrechts

  • Kiongozi wa NSW asema ukosefu wa utiifu, unaongeza idadi ya kesi jimboni
  • Wakaaji wa Victoria wapokea chanjo kwa wingi
  • Kesi mpya za Queensland zilikuwa katika karantini wakati zilikuwa katika hali ambukizi
  • Utawala wa Bidhaa na Tiba umetoa chanjo ya COVID-19 ya Moderna idhini ya muda

New South Wales
NSW imerekodi kesi mpya 356 ndani ya jamii, theluthi tatu kati yao walikuwa katika hali ambukizi ndani ya jamii. Wazee watatu ambao walikuwa hawaja chanjwa wame fariki, nakuongeza idadi ya vifo kupitia COVID-19 kufika 32 wakati wa mlipuko wa sasa.

Maeneo ya Byron Shire, Richmond Valley, Lismore na halmashauri ya jiji la Ballina kwa sasa ziko chini ya makatazo hadi saa sita dakika moja usiku wa Jumanne 17 Agosti 2021.

Kiongozi wa jimbo la NSW Gladys Berejiklian amesema ukosefu wa utiifu wa amri za afya ya umma, inaendelea kuwa sababu kubwa ya virusi kusambaa na amehamasisha kila mtu achanjwe.

Victoria
Victoria imerekodi kesi mpya 20 ndani ya jamii ambazo zina ungwa na milipuko inayo julikana, na ni kesi tano tu ambazo zilikuwa ndani ya karantini wakati zilikuwa katika hali ambukizi.

Waziri wa afya jimboni humo Martin Foley amesema, kuna idadi ya miadi za chanjo laki tatu elfu thelathini na tatu katika mwezi ujao.

Wakaaji wa Melbourne wanao elekea katika maeneo ya kanda, wanaweza pewa faini za takriban dola elfu tano, wakati idadi ya polisi 200 wametumwa kupiga doria katika barabara kuu naza vichochoro jimboni humo.

Hali ilivyokuwa nchini Australia katika masaa 24 yaliyo pita

Karantini, safari, zahanati za vipimo na malipo ya janga
Karantini na masharti ya vipimo yanasimamiwa nakutekelezwa na serikali zamajimbo na mikoa:

Kama unataka safiri nga'mbo, unaweza wasilisha ombi lako mtandaoni kupewa ruhusa. kwa taarifa ya ziada kuhusu masharti yakuondoka Australia. Kuna hatua za mpito kwa safari zakimataifa ambazo hufanyiwa tathmini mara kwa mara, na serikali pamoja nakuchapishwa kwenye tovuti ya .



Pata rasilmali zilizo tafsiriwa na huduma ya mawasiliano ya idara ya afya ya tamaduni nyingi jimboni NSW:


Zahanati za vipimo katika kila jimbo na mkoa:

 
 

Taarifa ya malipo ya janga katika kila jimbo na mkoa:

 
 

Share
Published 10 August 2021 4:44pm
By SBS/ALC Content
Presented by Gode Migerano
Source: SBS


Share this with family and friends